Senegal wataka kufika nusu fainali kombe la Dunia...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mashirika ya kimataifa
WAZIRI wa michezo wa Senegal, Matar Ba amesema timu ya taifa ya nchi hiyo itafanya vizuri zaidi katika michuano ya kombe la dunia zaidi ya taifa lolote la Afrika, kwa kufika nusu fainali ya michuano hiyo itayofanyika nchini Urusi mwakani.
Timu ya taifa ya Senegal

Mwaka 2002 kwa mara ya kwanza Senegal iliposhiriki michuano hiyo ilifanya vyema kwa kufika hatua ya robo fainali, Simba wa Teranga wamepangwa katika kundi H, na wakiwa na timu za Poland, Colombia na Japan.

"Tunapaswa kuwa na malengo yetu - malengo hayo ni kufikia nusu fainali na kufanya vizuri kuliko mwaka wa 2002," Waziri huyo aliiambia BBC.

Waziri Ba akasisitiza kwa kusema "Tuna timu nzuri na bora na tuna kocha wetu raia wa Senegal na tutajitayarisha vizuri kwa ajili ya kwenda kufanya vizuri.


Mchezo wa kwanza wa Senegal watacheza na Poland, June 19 kisha watacheza na Japan June 24, na watamaliza kazi kwa mchezo wa tatu kwa kukipiga na Colombia

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search