Watano wafariki, 11 wajeruhiwa...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

WATU watano wamefariki  na  11 wamejeruhiwa katika ajali kumi tofauti zilizotokea katika siku ya Krismass

Kamanda wa kikosi cha usalama barabarani SACP Fortunatus Musilimu akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Hayo yameelezwa leo jijini Dar es Salaam na Kamanda wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani SACP Fortunatus Musilimu akizungumza na waandishi wa habari alipokuwa akitoa taarifa ya tathimini ya hali ya ajali za barabarani nchini kuelekea mwishoni mwa mwaka 2017 na mwanzoni mwa mwaka 2018.

“Sikukuu ya Krismasi ya mwaka jana (2016) kulitokea jumla ya ajali 14 zilizosababisha vifo 10 na majeruhi 15, zinabainisha kuwepo kwa upungufu wa ajali 4 ambazo ni sawa na asilimia 29, upungufu wa vifo 5 ambavyo ni sawa na asilimia 50 na upungufu wa majeruhi 4 ambao ni sawa na asilimia 27,” amesema SACP Musilimu.

Amesema hata katika sikukuu ya kufungua zawadi (Boxing Day) Desemba 26, 2017 kulitokea ajali 6 nchini ambazo zilisababisha vifo 4 na majeruhi 8.

Ameeleza kuwa takwimu hizo zikilinganishwa na kipindi kama hicho kwa 2016 ambapo kulitokea ajali 6, vifo na majeruhi 9 zinabainisha kutokuwepo kwa ongezeko au upungufu wa ajali, kuwepo kwa upungufu wa kifo kimoja ambacho ni sawa na asilimia 20 na upungufu wa majeruhi mmoja ambaye ni sawa na asilimia 11.

SACP Musilimu ameongeza kuwa kuanzia Desemba 19, 2017 hadi Desemba 25, 2017 wiki moja kabla ya sikukuu ya krismas kulitokea ajali 42, vifo 46 na majeruhi 46.

Amesema takwimu hizo zikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka jana ambapo kulitokea ajali 55, vifo 52 na majeruhi 75 zinabainisha kuwepo kwa upungufu wa ajali 13 ambazo ni sawa na asilimia 24, upungufu wa vifo 6 ambavyo ni sawa na asilimia 12 na upungufu wa majeruhi 30 sawa na asilimia 39.

Amesema katika kipindi hiki ajali zimekuwa zikisababishwa na mwendo kasi, kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari (Overtaking), ulevi na magari mabovu.


Amewataka madereva kuhakikisha wanazingatia sheria wanapoendesha vyombo vya moto kwani ambao watakaidi watashurutishwa lakini pia watakamatwa na kuwekwa mahabusu na kisha kuwapeleka mahakamani pamoja na kuwafungia leseni zao wakitoka.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search