HESLB kuwasaka wadaiwa mikopo elimu ya juu...soma habari kamili na matukio360...#share

 Na Mwandishi Wetu,Dar es Salaam

BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu nchini (HESLB) imesema itaanza kuwasaka wanufaika  119,497 nchini ambao wamekiuka sheria ya kuanza kurejesha mikopo yenye thamani ya sh.bilioni 285.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo nchini (HSLEB) Abdul-Razaq Badru, akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi hiyo, Abdul-Razaq Badru  ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipokuwa akitoa tathmini ya utekelezaji ya majukumu ya bodi kwa mwaka wa fedha 2017/2018 ulioshia Desemba 31, 2017.

“Wanufaika hao ni wakuanzia mwaka 1994 hadi 1995 tutaanza kuwasaka kuanzia jumatatu januari 8, 2018,”amesema.

Amefafanua kuwa “Tutaanza kukagua taarifa za mishahara za waajiri (payroll) ili kubaini waajiri ambao wanawasilisha kiwango kidogo cha mikopo ya wafanyakazi wao ambao ni wanufaika pamoja na waajiri ambao hawawasilishi kabisa pesa hizo kwenye bodi hiyo kwa mujibu wa sheria ili wachukuliwe hatua stahiki,”amesema.

Amesema katika msako huo hawatamwacha mtu au mwajiri atakayekiuka sheria iliyoanzishwa na bodi na kufafanua kuwa sheria hiyo inatoa mamlaka ya kufanya ukaguzi na ni kosa kisheria kwa mtu yeyote kuzuia ukaguzi huo.

Amesema hadi Desemba 31,2017 sh bilioni 85 zilikusanywa huku lengo la makusanyo kwa mwaka mzima wa fedha utakaomalizika June 30 ,2018 ikiwa sh bilioni 130.


“Katika kazi hii ya ukusanyaji wa mikopo miezi hii sita tumewabaini wanufaika wapya 26000 na wameanza kulipa na kufanya jumla ya waliolipa kuwa zaidi ya sh 121,000,”amesema.

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search