Mkuu wa mkoa awasainisha mkataba wakuu wa wilaya....soma habari kamili na matukio360..#share
Na mwandishi wetu, Mbeya
MKUU wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amewasainisha mkataba wakuu wa wilaya ili watekeleze ujenzi wa vituo vya afya na zahanati 453 katika kata na vijiji kwa kipindi cha mwaka 2018/2020.
Amos Makalla
Mikataba hiyo imesainiwa leo mara baada ya kikao kazi cha kujadili
changamoto katika sekta ya afya kilichohusisha wakuu wa wilaya,
wakurugenzi wa halmashauri, waganga wakuu ,watendaji wa ngazi za kata na vijiji, na kwamba mikataba hiyo itapelekwa kwa Waziri wa Afya, Maendeleoya Jamii , Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.
Amesema kuwa amelazimika kufanya hivyo kutokana na mwamko duni wa ujenzi wa vituo vya afya na zahanati jambo linachangia jamii kukosa
huduma za afya ya msingi
"Wakuu wa wilaya hiki ni kipimo, utendaji wa kazi ni jambo la
kushangaza mkoa una vijiji 533 lakini vilivyo na vituo vya afya ni
233 sawa na asilimia 34.7 ambapo vijiji 300 havina huduma ya afya ,
wakati kuna kata 174 na zahanati zilizopo ni 25 kata 157 hazina kwa
kweli katika hili sitovumilia,"amesema Makalla
Makalla amesema watendaji wa serikali wanatakiwa kutambua sera inaelekeza nini katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.
Mwenyekiti wa wakuu wa wilaya , mkuu wa wilaya ya Chunya, Rehema
Madusa amesema watatekeleza haraka makubaliano ya mikataba hiyo kwa kuhakikisha wanatumia mapato ya ndani katika halmashauri na fedha zinazotoka serikalini ili ifikapo 2020 vituo vya afya na zahanati
vikamilike.
Mwenyekiti wa wakurugenzi wa halmashauri, Sophia Kumbuli amesema kuanzia sasa wataweka vipaumbele katika kutekeleza sera ya serikali kuwekeza katika sekta ya afya ili kuhakikisha changamoto ya upungufu vituo vya afya na zahanati inapungua.
Kaimu mganga mkuu wa mkoa, Yahya Msuya ametoa wiki mbili kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi kuandaa mpango kazi na kwamba uamuzi wa mkuu wa mkoa utasaidia kuboresha huduma za afya na idadi kubwa ya wananchi kupata huduma bora na salama.
MKUU wa mkoa wa Mbeya, Amos Makalla amewasainisha mkataba wakuu wa wilaya ili watekeleze ujenzi wa vituo vya afya na zahanati 453 katika kata na vijiji kwa kipindi cha mwaka 2018/2020.
Amos Makalla
Mikataba hiyo imesainiwa leo mara baada ya kikao kazi cha kujadili
changamoto katika sekta ya afya kilichohusisha wakuu wa wilaya,
wakurugenzi wa halmashauri, waganga wakuu ,watendaji wa ngazi za kata na vijiji, na kwamba mikataba hiyo itapelekwa kwa Waziri wa Afya, Maendeleoya Jamii , Jinsia Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu.
Amesema kuwa amelazimika kufanya hivyo kutokana na mwamko duni wa ujenzi wa vituo vya afya na zahanati jambo linachangia jamii kukosa
huduma za afya ya msingi
"Wakuu wa wilaya hiki ni kipimo, utendaji wa kazi ni jambo la
kushangaza mkoa una vijiji 533 lakini vilivyo na vituo vya afya ni
233 sawa na asilimia 34.7 ambapo vijiji 300 havina huduma ya afya ,
wakati kuna kata 174 na zahanati zilizopo ni 25 kata 157 hazina kwa
kweli katika hili sitovumilia,"amesema Makalla
Makalla amesema watendaji wa serikali wanatakiwa kutambua sera inaelekeza nini katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora.
Mwenyekiti wa wakuu wa wilaya , mkuu wa wilaya ya Chunya, Rehema
Madusa amesema watatekeleza haraka makubaliano ya mikataba hiyo kwa kuhakikisha wanatumia mapato ya ndani katika halmashauri na fedha zinazotoka serikalini ili ifikapo 2020 vituo vya afya na zahanati
vikamilike.
Mwenyekiti wa wakurugenzi wa halmashauri, Sophia Kumbuli amesema kuanzia sasa wataweka vipaumbele katika kutekeleza sera ya serikali kuwekeza katika sekta ya afya ili kuhakikisha changamoto ya upungufu vituo vya afya na zahanati inapungua.
Kaimu mganga mkuu wa mkoa, Yahya Msuya ametoa wiki mbili kwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi kuandaa mpango kazi na kwamba uamuzi wa mkuu wa mkoa utasaidia kuboresha huduma za afya na idadi kubwa ya wananchi kupata huduma bora na salama.
About Author Matukio360
Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.
No comments:
Post a Comment