Uminywaji uhuru kujieleza LHRC kushtaki kimataifa...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara,Dar es Salaam

KUTOKANA na mbano wa uhuru wa kujieleza nchini, Kituo cha Sheria na Haki za Binadam (LHRC), kimesema kinampango wa kushtaki suala hilo kwenye vyombo vya kimataifa vinavyohusika na uangalizi wa haki za binadamu.
Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Dk. Helen Kijo-Bisimba, akizungumzi na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Msimamo huo umetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC Dk. Helen Kijo-Bisimba akizungumza na waandishi wa habari siku moja baada ya ya Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) kuvitoza vituo vitano vya televisheni faini ya sh. milioni 60.

“Tumeshuhudia serikali kupitia TCRA ikitoa adhabu kwa vituo vitano vikubwa vya luninga ambavyo nia Azam TV, ITV, Channel 10, Str TV na EATV kwa kile kinachodaiwa kuwa ni ukiukwaji wa kanuni ya maudhui 2005 baada ya televisheni hizo kurusha habari kuhusu tathmini ya haki za binadamu katika uchaguzi mdogo wa madiwani uliofanyika Novemba 2017 iliyotolewa na LHRC,” amesema Dk. Kijo-Bisimba.

Ameongeza “LHRC imechukua hatua ya kutoa taarifa kwa vyombo vya kimataifa vinavyohusika na uangalizi wa haki za binadamu kuomba waingilie kati suala la uhuru wa kujieleza nchini,”

Dk. Kijo-Bisimba amesema kufuatia hatua hiyo ya TCRA, LHRC imechukua hatua nyingine nne za kufanya ambazo ni kuandika barua TCRA kuwataka kufanya semina kwa kituo hicho na taasisi nyingine juu ya namna bora ya kuandaa maudhui.

Nyingine ni kuungana na wadau ambao wako tayari kwenda mahakamani kuomba tafsiri ya neno UCHOCEZI na baadhi ya vifungu vya kanuni ya maudhui hususani kifungu namba 8 katika mazingira ya utawala wa serikali dhidi ya raia.

Kimeanzisha harambee ya kuchangia gharama ya kuvisaidia vyombo vya habari vilivyokumbwa na adhabu pamoja na kuitaka serikali ya awamu ya tano kuheshimu katiba iliyopo kwa kutoingilia uhuru wa kujieleza.


Kwa mujibu wa kamati ya maudhui ya TCRA, vyombo hivyo vimetiwa hatiani kwa makosa matatu chini ya kifungu cha 5 na 6 vya kanuni za maudhui za mwaka 2005 na kupigwa faini kwa viwango tofauti pamoja na kuwekwa chini ya uangalizi kwa miezi sita.  

About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search