Waziri aagiza waliokula fedha za Tasaf wafikishwe mahakamani...soma habari kamili na matukio360...#share

Na mwandishi wetu, Mbeya.
UONGOZI wa Mkoa wa Mbeya umeagizwa kufuatilia sh milion 32
zilizotolewa kimakosa kwa kaya 20 kupitia mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) na watakaoshindwa kurejesha wafikishwe mahakamani.
Waziri George Mkuchika
Agizo hilo limetolea na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika, baada ya kupata taarifa ya jumla ya kaya 54 zenye sifa kukosa ruzuku huku fedha nyingi zikilipwa kwa kaya zisizo na sifa.
"Nasikitishwa na kaya zilizoondolewa kwenye mpango kutochukuliwa hatua zozote. Hili halikubaliki ni lazima fedha zirejeshwe ili zisaidie kaya ambazo hazikuingizwa kwenye mpango," amesema Mkuchika
Katibu Tawala Mkoa, Mariam Mtunguja amesema katika awamu ya pili na tatu ya mradi mkoa huo uliopokea zaidi ya sh bilioni 9 kwa ajili ya
kutekeleza miradi 379.
Amesema hadi sasa tangu mpango huo uanze mkoa umetumia zaidi ya
sh bilioni 26.7 katika awamu 15 na jumla ya kaya 42,000 zimenufaika, kati ya fedha hizo sh bilioni 3 zimetumika katika ufuatiliaji.
Mratibu Tasaf wa jiji hilo, Emmanuel Kimbe amesema kuna miradi 77 ikiwemo ya afya, elimu, miundombinu na makundi maalumu yenye thamani ya sh bilioni 2.8
UONGOZI wa Mkoa wa Mbeya umeagizwa kufuatilia sh milion 32
zilizotolewa kimakosa kwa kaya 20 kupitia mfuko wa Maendeleo ya Jamii(TASAF) na watakaoshindwa kurejesha wafikishwe mahakamani.
Waziri George Mkuchika
Agizo hilo limetolea na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya
Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Mkuchika, baada ya kupata taarifa ya jumla ya kaya 54 zenye sifa kukosa ruzuku huku fedha nyingi zikilipwa kwa kaya zisizo na sifa.
"Nasikitishwa na kaya zilizoondolewa kwenye mpango kutochukuliwa hatua zozote. Hili halikubaliki ni lazima fedha zirejeshwe ili zisaidie kaya ambazo hazikuingizwa kwenye mpango," amesema Mkuchika
Katibu Tawala Mkoa, Mariam Mtunguja amesema katika awamu ya pili na tatu ya mradi mkoa huo uliopokea zaidi ya sh bilioni 9 kwa ajili ya
kutekeleza miradi 379.
Amesema hadi sasa tangu mpango huo uanze mkoa umetumia zaidi ya
sh bilioni 26.7 katika awamu 15 na jumla ya kaya 42,000 zimenufaika, kati ya fedha hizo sh bilioni 3 zimetumika katika ufuatiliaji.
Mratibu Tasaf wa jiji hilo, Emmanuel Kimbe amesema kuna miradi 77 ikiwemo ya afya, elimu, miundombinu na makundi maalumu yenye thamani ya sh bilioni 2.8
About Author Matukio360
Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.
No comments:
Post a Comment