Bilioni moja kununua mashine ya vinasaba....soma habari kamili na matukio360....#share
Na Mwajuma Juma, Zanzibar
SHILINGI bilioni moja zimetengwa kununua mashine ya kuchunguza vinasaba DNA visiwani Zanzibar.
Mahmoud Thabit Kombo
SHILINGI bilioni moja zimetengwa kununua mashine ya kuchunguza vinasaba DNA visiwani Zanzibar.
Mahmoud Thabit Kombo
Hayo yameelezwa na Waziri wa afya, Mahmoud Thabit Kombo wakati akijibu swali la mwakilishi wa jimbo la Chake Chake Suleiman Sarhani aliyetaka kujua mchakato wa ununuzi wa mashine hiyo umefikia wapi.
Amesema ili kufanikisha hilo tayari serikali imeshatangaza zabuni kwa ajili ya ununuzi wa mashine hiyo ambayo ni ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kutambua matukio mbali mbali ikiwemo vitendo vya ukatili wa kijinsia na ubakaji.
“Mheshimiwa Spika mashine hiyo itakuwa ni ya kisasa na ina uwezo wa kugundua au kukamua maji maji ya mtu aliyebakwa kwa muda wa wiki moja tokea kitendo kufanyika ikiwa hakusafishwa,” amesisitiza.
Amesema ili kufanikisha hilo tayari serikali imeshatangaza zabuni kwa ajili ya ununuzi wa mashine hiyo ambayo ni ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kutambua matukio mbali mbali ikiwemo vitendo vya ukatili wa kijinsia na ubakaji.
“Mheshimiwa Spika mashine hiyo itakuwa ni ya kisasa na ina uwezo wa kugundua au kukamua maji maji ya mtu aliyebakwa kwa muda wa wiki moja tokea kitendo kufanyika ikiwa hakusafishwa,” amesisitiza.
Amesema tayari mkemia mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar amefanya safari nchini Kenya kwa ajili ya kuangalia sampuli ya mashine hiyo na kufanya mazungumzo na wakala wake.
No comments:
Post a Comment