CUF wataka wazee, viongozi wa dini na wastaafu wakutane na Magufuli....soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara, Dar es Salaam

CHAMA cha Wananchi CUF kimewataka wazee, viongozi wa stahafu na viongozi wa dini akiwamo Kadinali Polycarp Pengo wamshauri na kumpa nasaha rais John Magufuli arudi kwenye mstari ili kulinusuru taifa na mwelekeo mbaya unaolikabili.
Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi CUF, Julius Mtatiro akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mwelekeo huo mbaya umetajwa kuwa ni kushamiri kwa mauji, utekaji na mashabulizi, mashambulizi dhidi ya demokrasia, mihimili ya dola kuwekwa mfukoni mwa serikali, hali ya uchumi wa nchi na kuvunjwa kwa haki na kukithiri kwa vitendo vya upendeleo.

Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi wa CUF Julius Mtatiro alipokuwa akitoa taarifa zinazoeleza kuwepo kwa mwelekeo mbaya wa taifa na kuishauri serikali.

“Taifa letu linao wazee, linao waasisi, linao viongozi wastaafu. Kwa sababu mambo hayako sawa kwenye nchi yetu, wazee wetu Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Warioba, Butiku na wengine wote simameni na mwambieni JPM arudi kwenye mstari,”

“Hakuna mtanzania ambaye angelipenda kupoteza muda wake kumkosoa rais na serikali yake, lakini watanzania wanawajibika kufanya hivyo kwa sababu ya maamuzi ya rais na utendaji wa serikali yake vinaathari za moja kwa moja kawa maisha ya kizazi chetu na kijacho,” amesema na kuongeza Mtatiro.

Mauaji, utekeji na mashambulizi
Mtatiro amesema kuwa vitendo hivyo kwa sasa nchini ni mambo ya kawaida. Ameeleza kwamba matukio hayo leo yakutisha ya mauaji yamelitia madoa  ya damu serikali lakini hadi sasa vyombo vyenye dhamana havina majibu ya matukio hayo.

Mashambulizi dhidi ya Demokrasia
Amesema tangu kuingia madarakani kwa uongozi wa serikali ya awamu ya tano, kumekuwa na jitihada kubwa za kuua demokrasia na mfumo wa vyama vingi hapa nchini na amedai kuwa juhudi hizo zinafanywa na rais Magufuli.

Mihimili ya dola Kuwekwa mfukoni mwa serikali
Mwenyekiti huyo wakamati ya uongozi amedai kuwa mhimili mmoja (serikali) umejipa mamlaka makubwa kiasi cha kudhibiti mihimili mingine. Ametoa mfano kwa kusema serikali kwa sasa inapanga mipango mingi na inatumia fedha nyingi za taifa bila kulihusisha bunge. Hivyo imelidhibiti bunge na mahakama pia imedhibitiwa.

Hali ya uchumi wa nchi
Amedai, hali ya uchumi kwa sasa inaanguka kutokana na kwamba mzunguko wa fedha ni mdogo, hali mbaya ya biashara, mfumuko wa bei za bidhaa za vyakula na mabenki kufungwa, hivyo amesema kama hatua isipochukuliwa taifa litaenda kubaya.

Kuvunjwa kwa haki na kukithiri kwa vitendo vya upendeleo.
Amesema utawala wa awamu hii chini ya rais Magufuli unaongoza taifa kwa kuwa na “double standard”, kujuana na upendeleo ambapo alitoa mfano wa bamoa bomoa iliyowafanya kwa wakazi wa kimara jijini Dar es Salaam kwa madai ya kuvamia hifadhi ya barabara huku juzi rais akisitisha bomoa bomoa kwa wakazi wa Mwanza waliovamia eneo la uwanja wa ndige.



About Author Matukio360

Matukio360 ni sehemu pekee inayokuletea matukio ya moto moto kutoka pande zote za dunia katika wakati ule ule yalipotokea yaani mubashara. Habari ni za uhakika na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na kuandikwa kwa ueledi mkubwa na sio ukanjanja. Usibanduke katika ukurasa huu wa Matukio360, wajulishe na marafiki zako sasa wajipatie habari za uhakika.

No comments:

Post a Comment

Leo leo Plus

Start typing and press Enter to search