Chadema waituhumu CCM kucheza rafu uchaguzi Kinondoni...soma habari kamili na matukio360...#share

Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
CHAMA cha Chadema kimedai kuwa baadhi ya viongozi wa CCM Kinondoni wanapita nyumba kwa nyumba kununua na kuandika namba za shahada za kupigia kura za wananchi na kuwadanganya hazitatumika na watapewa nyingine.
Pia kimemtuhumu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuwa anafanya hujuma za kutaka kuibeba CCM ili ishinde katika uchaguzi wa marudio ya Ubunge wa Februari 19,2018.
Pia kimemtuhumu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuwa anafanya hujuma za kutaka kuibeba CCM ili ishinde katika uchaguzi wa marudio ya Ubunge wa Februari 19,2018.
Mkuu wa Operesheni wa Uchaguzi Chadema Benson Kigaila akizungumza na waandishi wa habari juu ya mwenendo wa uchaguzi mdogo wa ubunge Kinondoni.
Kufuatia vitendo hivyo kitaandika barua ya malalamiko kwenda Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kuhusu njama hizo.
Kimetoa tuhuma hizo leo jijini Dar es salaam katika mkutano wake na waandishi wa habari kuelezea mwenendo mzima wa uchaguzi Jimbo la Kinondoni na kuwa wanamshutumu Mkurugenzi wa halmashauri ya Kinondoni, Aron Kagurumjuli kwa kuiandikia Chadema barua mbili ikilalamikiwa kuvunja kanuni za maadili ya uchaguzi katika kampeni zao.
Kimetoa tuhuma hizo leo jijini Dar es salaam katika mkutano wake na waandishi wa habari kuelezea mwenendo mzima wa uchaguzi Jimbo la Kinondoni na kuwa wanamshutumu Mkurugenzi wa halmashauri ya Kinondoni, Aron Kagurumjuli kwa kuiandikia Chadema barua mbili ikilalamikiwa kuvunja kanuni za maadili ya uchaguzi katika kampeni zao.
Mkuu wa Operesheni ya Uchaguzi wa
Chadema Benson Kigaila amesema katika barua ya kwanza wanalalamikiwa na mtu
asiyejulikana kuwa Januari 28, 2018 walifanya kampeni ya nyumba kwa nyumba na
maandamano nje ya muda uliopangwa enrollment la Kigogo kuanzia Mbuyuni mpaka Baa ya Londor badala
ya Ndugumbi Mikoroshini.
“Na katika barua ya
pili tunalalamikiwa na chama cha CUF Lipumba, kuwa tunatumia salamu za CUF
kwenye jukwaa letu, tunaweka bendera ya CUF katika jukwaa letu, viongozi wa CUF
kukaa katika meza kuu ya viongozi na kupanda katika jukwaa letu na kuwatumia
viongozi wa CUF kupita nyumba hadi nyumba wakiomba kura huku wakiwa wamevaa
sare za CUF,” amesema Kigaila.
Kigaila amedai tuhuma hizo ni za kutengenezwa za uongo na kwamba
kama ni kampeni walifanya kweli Kigogo kama ratiba ilivyokuwa inasema na
hawakutakiwa kuwa Ndugumbi kama inavyodaiwa.
“CCM hawachaguliki
kinondoni, walishalikoroga kwa kumteua Maulid Mtulia aliyeukana ubunge, wanakinondoni wameshachukia hilo, hivyo haya ni maelekezo ambayo
wakurugenzi walipewa kuhakikisha CCM inashinda,” amesema Kigaila.
Katika hatua nyingine kampeni meneja wa Salum
Mwalimu, Said Kubenea amesema mkurugenzi huyo amekuwa akiwachezea kwani
alishawahi kufanya hivyo katika uchaguzi wa Meya wa Kinondoni na kuapa kuwa
hawatakubali tena kuchezewa.
Kwa upande mwingine
Kubenea amedai kuwa CCM inapita nyumba kwa nyumba kununua na kuandika namba
za shahada za kupigia kura kwa wananchi wakiwadanganya kuwa hazitatumika na watapewa nyingine.
Amesema lengo la
kufanya hivyo ni kutaka kupunguza idadi ya kura ili waweze kupenyeza kura zao
siku ya uchaguzi.
Hivyo amewataka kuacha
mara moja kufanya hivyo kwani wakiendelea watatuma vijana wao kwa ajili ya
kulifuatilia jambo hilo ili kulizuia.
No comments:
Post a Comment