Makonda awasaka waliopora mali za Bakwata Dar es salaam....soma habari kamili na matukio360....#share

Na Salha Mohamed, Dar es Salaam
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amelitaka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania(BAKWATA) mkoani humo kumpa orodha ya maeneo ya baraza yaliyoporwa mkoani humo.
Pia amewataka wamuombee kwa M/Mungu ili aweze kuwasaidia watu na kupata haki zao.
Paul Makonda akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi wa majengo ya makao makuu ya Bakwata leo jijini Dar es salaam
Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa makao makuu ya baraza hilo na shule yanayogharimu sh bilioni 4.5
"Ninaomba mniletee orodha ya maeneo ya Bakwata ya Dar es Salaam yaliyoporwa nataka kushughulika nayo ambayo wajanja wajanja wameyaingilia, "amesema.
Amewahakikishia maeneo hayo yatapatikana ili waislamu wafanye mambo yao ya maendeleo.
Katika hatua nyingine Makonda amewataka waumini wa madhehebu yote nchini kuwathamini viongozi wao bila kusubiri kuombwa msaada.
Kwa upande wake Mufti wa Tanzania, Abubakar Zuberi amesema "Tunakuombea kwa Mungu... Awali Bakwata kulikuwa kunafitina ndani kwa ndani na nje pia ndiyo maana hakukuwa na maendeleo kwa miaka zaidi ya 50".
Amewataka waislamu wajitambue, wabadilike na kuacha mazoea na kutengeneza dhambi kwa kuweka vigenge kwa kufanya fitina.
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amelitaka Baraza Kuu la Waislamu Tanzania(BAKWATA) mkoani humo kumpa orodha ya maeneo ya baraza yaliyoporwa mkoani humo.
Pia amewataka wamuombee kwa M/Mungu ili aweze kuwasaidia watu na kupata haki zao.
Paul Makonda akizungumza mara baada ya kukagua ujenzi wa majengo ya makao makuu ya Bakwata leo jijini Dar es salaam
Ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam alipotembelea kukagua maendeleo ya ujenzi wa makao makuu ya baraza hilo na shule yanayogharimu sh bilioni 4.5
"Ninaomba mniletee orodha ya maeneo ya Bakwata ya Dar es Salaam yaliyoporwa nataka kushughulika nayo ambayo wajanja wajanja wameyaingilia, "amesema.
Amewahakikishia maeneo hayo yatapatikana ili waislamu wafanye mambo yao ya maendeleo.
Katika hatua nyingine Makonda amewataka waumini wa madhehebu yote nchini kuwathamini viongozi wao bila kusubiri kuombwa msaada.
Kwa upande wake Mufti wa Tanzania, Abubakar Zuberi amesema "Tunakuombea kwa Mungu... Awali Bakwata kulikuwa kunafitina ndani kwa ndani na nje pia ndiyo maana hakukuwa na maendeleo kwa miaka zaidi ya 50".
Amewataka waislamu wajitambue, wabadilike na kuacha mazoea na kutengeneza dhambi kwa kuweka vigenge kwa kufanya fitina.
No comments:
Post a Comment