UPDATES: Sugu, Masonga jela miezi mitano....soma habari kamili na matukio360...#share
Na mwandishi wetu, Mbeya
MAHAKAMA ya hakimu mkazi Mbeya leo imewatia hatiani Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi na katibu wa Chadema nyanda za juu kusini Emmanuel Masonga na kuwahukumu kifungoni cha miezi mitano jela
Wamehukumiwa kwa kosa la kumtumia lugha ya fedheha dhidi ya rais John Magufuli. Hukumu imetolewa na hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo , Michael Mteite.
Awali kabla ya hukumu ulinzi uliimarishwa katika Mahakama hiyo na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU)
MAHAKAMA ya hakimu mkazi Mbeya leo imewatia hatiani Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi na katibu wa Chadema nyanda za juu kusini Emmanuel Masonga na kuwahukumu kifungoni cha miezi mitano jela
Wamehukumiwa kwa kosa la kumtumia lugha ya fedheha dhidi ya rais John Magufuli. Hukumu imetolewa na hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo , Michael Mteite.
Awali kabla ya hukumu ulinzi uliimarishwa katika Mahakama hiyo na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU)
Wawili hao wanadaiwa kutenda kosa hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 30,2017 eneo la Uwanja wa Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.
.
Upande wa mashtaka na wa utetezi ulikamilisha ushahidi Februari 9,2018.
Upande wa mashtaka na wa utetezi ulikamilisha ushahidi Februari 9,2018.
Jamhuri iliwasilisha mashahidi watano na kielelezo kimoja cha sauti iliyodaiwa kurekodiwa na shahidi wa tano, Inspekta Joram Magova.
Upande wa utetezi uliwasilisha mashahidi sita wakiwamo Sugu na Masonga waliokana kutamka maneno wanayoshtakiwa kuyatoa.
Washtakiwa walitetewa na mawakili Sabina Yongo, Boniface Mwabukusi na Hekima Mwasipu kabla ya kujitoa, hivyo sasa wanawakilishwa na Peter Kibatala.
Kwa mara ya kwanza, Sugu na Masonga walifikishwa mahakamani Januari 16 na kusomewa mashtaka na Wakili wa Serikali Mkuu, Joseph Pande aliyeeleza upelelezi ulikuwa umekamilika na walikuwa tayari kuendelea na usikilizaji
No comments:
Post a Comment