Manispaa ya Ilala yaokoa sh.bilioni 1.5 kwa kipindi cha Januari hadi Machi, 2018...soma habari kamili na matukio360..#share

Na Abraham Ntambara,
Dar es Salaam
HALMASHAURI ya Manispaa
ya Ilala jijini Dar es Salaam imeokoa sh.bilioni 1.5 kwa kipindi cha kuanzia
mwezi Januari hadi Machi 2018 kutokana na kushinda kesi saba.
Hayo yamebainishwa leo
jijini Dar es Salaam na Kaimu
Mwenyekiti wa kamati ya fedha na utawala, Waziri Mweneviale alipokuwa akisoma
taarifa ya utekelezaji wa majukumu ya kamati hiyo kwa robo mwaka ya kipindi
hicho mbele ya Baraza la Madiwani na kujadiliwa.
Taarifa nyingine za Utekelezaji wa
Majukumu zilizosomwa mbele ya Baraza hilo na kujadiliwa ni za kamati ya Fedha,
Uchumi na Huduma za jamii pamoja na kamati ya Mipango Miji na Mazingira.
“Halmashauri imefanikiwa kushinda kesi
takribani saba ikiwemo kesi Na. 54/2003 kati ya Charles Moses dhidi ya
Halmashauri ya Manispaa ya Ilala ambapo mdai alikuwa akiidai halmashauri kiasi
cha Tsh 1,500,000,000 hivyo kwa kipindi hicho kamati imeokoa kiasi hicho cha
fedha,” amesema Mweneviale.
Ameeleza kuwa kwa kipindi hicho kamati
imefanikiwa kusimamia mapato na matumizi ya halmashauri ambapo imeweza
kukusanya jumla ya sh.10,348,333,506 sawa na asilimia 88 ya makisio ya sh.11,793,447,388.50
bila kuweka kodi ya majengo ya sh 800,000,000.00 ambazo zinakusanywa na
Serikali kuu .
Mwenenviale ameongeza kwamba kamati
hiyo imeidhinisha matumizi ya force account kwa ajili ya ujenzi wa ukuta wa
pavement katika hospitali ya Mama na Mtoto Chanika kwa gharama ya sh.183,864,091.20.
Amebainisha kuwa kamati hiyo imeweza
kusimamia uchangiaji wa mapato ya ndani kwenye miradi ya Maendeleo kwa asilimia
60% na kwamba halmashauri ilichangia jumla ya shilling 3,900,000 kwenye Akaunti
ya Maendeleo ikiwa ni sawa na asilimia 80% ya kiasi kilichopangwa kwa kipindi
hicho cha January hadi Machi.
Kwa upande wa taarifa ya kudumu ya kamati ya Uchumi na
huduma za jamii iliyosomwa na Kaimu Mwenyekiti, Helen Lyatula, amesema kamati
hiyo imefanikiwa kwa kipindi hicho kusimamia utekelezaji wa shughuli mbali
mbali za miradi ya maendeleo.
Amesema moja ya miradi waliyosimamia ni taaluma na
nidhamu katika shule zote za awali na msingi za serikali na zisizo za serikali,
kutoa muongozo na taratibu mbalimbali za kufanikisha malengo waliyoweka
kulingana na sera ya elimu na kuongeza kwamba inatarajiwa jumla ya walimu 1653 wa
shule ya msingi watapandishwa vyeo na madaraja.
“Jumla ya walimu 1653 wa shule ya msingi
wanatarajia kupandishwa vyeo na madaraja, lakini halmashauri pia imepokea
vitabu 100, 904 toka TAMISEMI na kusambaza kwa shule zote msingi,” amesema
Lyatula.
Aidha amesema pamoja na mafanikio waliyoyapata bado kumekuwepo na changamoto zinazokabili idara na vitengo katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa madai ya likizo hadi sasa jumla ya walimu wa shule za msingi 1837 wanadai kiasi cha sh 478,346,684,00, pamoja na ukomo wa bajeti katika utekelezaji shughuli mbalimbali za kilimo, ushirika na umwagiliaji.
Aidha amesema pamoja na mafanikio waliyoyapata bado kumekuwepo na changamoto zinazokabili idara na vitengo katika utekelezaji wa majukumu yake ya kila siku ikiwa ni pamoja na kuwepo kwa madai ya likizo hadi sasa jumla ya walimu wa shule za msingi 1837 wanadai kiasi cha sh 478,346,684,00, pamoja na ukomo wa bajeti katika utekelezaji shughuli mbalimbali za kilimo, ushirika na umwagiliaji.
Naye Kaimu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya
Mipangomiji na Mazingira Greyson Siwilwa, akisoma taarifa ya kamati hiyo
amesema kwa kipindi hicho imeweza kusimamia utekelezaji wa shughuli mbali za
uendeshaji wa miradi ya maendeleo kupitia Idara ya Mipangomiji na Ardhi,
Ujenzi, Maji na Uthabiti wa Maji Taka na
Uhifadhi wa Mazingira na Udhibiti wa taka ngumu.

No comments:
Post a Comment